Michezo

Messi: Nitaendelea kubaki Barcelona sio kwamba napenda ila rais ameniambia njia pekee ya kuondoka ni kulipa € 700m, na hiyo haiwezekani

Mshambuliaji hatari wa Club ya FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina  Lionel Messi ameweka wazi juu ya kile alichozungumza mwanzo kuwa anataka kuondoka Barcelona  msimu ujao, akifanya mahojiano na chombo kimoja cha habari Messi alisema haya:

“Niliiambia klabu na Rais wa klabu kwamba ninataka kuondoka. Nimekuwa nikimwambia mwaka mzima, Ukweli ni kwamba hakuna mikakati endelevu katika klabu hii. Wanaziba tu mashimo kipindi matatizo yanapotokea. Siwezi kuingia vita dhidi ya klabu ya maisha yangu. Nitabaki”.

“Niliiambia klabu, Rais, kwamba ninataka kuondoka. Nimekuwa nikimwambia mwaka mzima. “Ukweli ni kwamba hakuna mikakati endelevu katika klabu hii. Wanaziba tu mashimo kipindi matatizo yanapotokea. Siwezi kuingia vita dhidi ya klabu ya maisha yangu. Nitabaki”.

“Sina furaha na nilitaka kuondoka. Sijaruhusiwa kwa njia yoyote na nitaendelea kubaki klabuni ili nisiingie kwenye mgogoro wa kisheria (mahakamani) na klabu ya ndoto zangu. Uongozi wa klabu unaoongozwa na Bartomeu ni janga.”

Nitaendelea kubaki katika klabu hii kwa sababu rais aliniambia kuwa njia pekee ya kuondoka ni kulipa kifungu cha € 700m, na hiyo haiwezekani.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents