Michezo

Messi vs Ronaldo; Nani atakaye maliza maisha ya soka akiwa na magoli mengi zaidi ya mwenzie?

Hakuna ubishi kuwa tupo katika zama za Lionel Messi na Cristiano Ronaldo katika mchezo huu pendwa wa soka, na ushindani kati ya nyota hawa wawili ni mkubwa mnoo ndani ya uwanja na hata nje kwa mashabiki wakishindwa kumpata mbora zaidi ya mwingine lakini hii ikisababishwa na rekodi wanazoweka kila uchwao na huwenda kikawa kizazi cha mwisho na bora kwa muda wote katika kabumbu.
Image result for Josef Biscan goals
Ukiachiambali mataji ambayo wamekuwa wakiendelea kushinda kila siku, lakini wote bado wanaonekana kuwa wanaendelea kuwa na mvutano mkubwa licha ya kuwa kwa sasa wakicheza ligi tofauti na bado kuwacha maswali mengi kwa wapenzi wa soka, je ninani atakayemaliza maisha ya soka akiwa na mabao mengi zaidi ya mwingine.
Cristiano aliweza kufikisha jumla ya mabao 700 usiku wa kuamkia leo Jumanne Oktoba 15, 2019 dhidi ya Ukraine kwenye mchezo wa kufuzu michuano ya Euro huku akitimiza jumla ya mechi 973 wakati wakitofauitiana kidogo na hasimu wake Muargentina, Lionel Messi ambaye ana jumla ya magoli 668 akiwa nyuma kwa magoli 32 dhidi ya Mreno huyo wakati mpaka sasa amecheza michezo 823.
Image result for Josef Biscan goals

Kwa upande mwingine watu wanamtazamia, Messi kama ananafasi kubwa zaidi ya hasimu wake Ronaldo kutokana na kuwa na umri mdogo wa miaka 32 dhidi ya 35 aliyokuwa nayo Mreno licha ya nyota huyo wa Juventus kukusudia kulitumikia soka mpaka atakapo fikisha miaka 40 ndipo atakapotundika daluga.

Mara kadhaa, Messi amekuwa akisumbuliwa na majeraha na hivyo kusababisha kupunguza spidi yake ya upachikaji mabao lakini bado amekuwa akiendelea rekodi zake mwenyewe.

Akicheza michezo 31 ndani ya klabu ya Sporting CP, na kufunga mabao matano 5,  magoli 118 katika mechi 292  Manchester United, Ronaldo aliendeleza moto wake huko Hispania baada ya kuifungia Real Madrid magoli 451 kwenye michezo 438 aliyoshuka uwanjani na kwa sasa kiumbe huyo anafanya yake pale Turin, ashafunga mabao 32 katika mechi 51.

Kwa tafsri nyepesi tu, kiumbe huyu ana asilimia 47 ya kufunga bao kila dakika  112 kwenye michezo aliyocheza na kwa sasa anakimbizia rekodi ya mchawi wa soka Muaustralia, Josef Biscan aliyefunga magoli 805.

By Hamza Fumo

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents