Habari

Meya Mwita akanusha kudaiwa kuhama Chadema

Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amekanusha uvumi kuhusu kudaiwa kutaka kuhama chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema habari hizo si za kweli hivyo ameomba taarifa hizo kupuuzwa.

Taarifa iliyotolewa leo na Ofisa Habari na Msemaji Mkuu wa Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam, Christina Mwagala imeeleza kuwa Mstahili Meya huyo hajawahi kudhani wala kufikiria kuhama chama hicho.

Ndugu waandishi wa habari: Nimeshikwa na mshtuko, simanzi baada ya kusambaa kwa taarifa ambazo naweza kusema kuwa ni za uzushi kwamba nina mpango wa kujiondoa ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema. naomba taarifa hizo zipuuzwe maana hazina ukweli wowote na kwamba zinampango wa kunichafua mimi pamoja na Chama Changu.

Ndugu wandishi wa habari : Napenda ieleweke kuwa sijawahi kudhani wala kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote kile cha siasa. Chadema ni chama ambacho nimetoka nacho mbali tangu mwaka 2004 hadi leo, nimejenga chama kwa gaharama zangu mwenyewe.

Ndugu waandishi wa habari: Leo nimekuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam kupitia Chama Changu cha Chadema,natambua kuwa chama kimeniheshimu sana kwa kunipa nafasi hii hivyo sina sababu ya kuondoka kwani ninania ya kuwatumikia Wananchi ambao wameniamini na wamenichagua kwa mapenzi yao wakiamini kuwa nitawaletea Maendeleo nikiwa ndani ya Chama Cha Chadema.

.Nafahamu tuhuma hizi zinatokana na aina ya utendaji wangu katika Jiji la Dar es Salaam kwani nimekuwa nikifanya kazi badala ya kupambana na serikali pale ambapo watu wanaamini kuwa mambo hayajaenda sawa.

Ndugu waandishi wa habari: Kukaa kwangu kimya huku ,kutokufanya siasa za kiharakati ndani ya jiji la Dar es Salaam haimanishi kwamba nipo upande wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi nasio kufanya harakati za kisiasa kwakuwa nina nia ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Ndugu waandishi wahabari: Naomba ifahamike kuwa hakuna Mkurya ambaye aliwahi kuwa msaliti,katika nafasi yoyote ambayo aliwahi kuwa nayo. Kutokana historia hiyo, naomba niaminike na wanachama na wananchi wote kuwa haitakuja kutokea Mkurya mimi nikakisaliti chama changu.

Nakama itakuja kutokea nikafanya hivyo ninaweza kuhatarisha maisha yangu, Familia yangu, na hivyo kujikuta nikaingia kwenye matatizo makubwa ambayo kimsingi sio mazuri. Mama yangu ni mjane, kama itafanya hivyo Chadema wote Mkoa wa Mara hawawezi kuwaacha ndugu zangu salama .

Ndugu waandishi wa habari : Tangu nimeona watu wote waliohama ,kusaliti vyama vyao, maisha yao yamekuwa mabaya, nahata imani kwa Wananchi wao imepungua. Hivyo na Mimi sitaki kuwa kama wao, ninania ya dhati ya kukitumikia chama changu kwa uaminifu mkubwa kama ambavyo wao wameniamini.

Kuliko kuhama Chadema ni heri mkanitafutie Mahala pengine pakuishi ambapo itakuwa ni mbinguni lakini sio hapa duniani ama kwenda kwenye Chama kingine chochote cha kisisasa. Kikubwa napenda kuwaeleza wana chama wote wa Chadema kuwa hivi sasa kila mmoja tujielekeze kwa nguvu zetu zote kwenye kampeni hivi za uchaguzi mdogo wa madiwani unaotarajiwa kufanyika Novemba 26 mwaka huu.msikubali kutolewa kwenye maandalizi ya uchaguzi.

Imetolewa leo Novemba 23/2017
Christina Mwagala, Ofisa Habari na Msemaji Mkuu wa Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents