Meya Sitta afunga maadhimisho ya Siku ya Mvuvi kwa namna ya kipekee
Meya wa Kinindoni Benjamin Sitta Serikali imesema inampango mkakati mzuri katika kuliendeleza sekta ya uvuvi kufika mbele zaidi na kutoa ajira za uhakika kwa Watanzania ambao wanafanya shughuli hiyo.
Meya amesema hayo akiwa Msasani Soko la Samaki wakati akifunga maadhimisho ya Siku ya Mvuvi ambayo iliambatana na utoaji wa zawadi kwa wavuvi waliofanya vizuri katika mashindano yakuvua samaki kwa vitumbwi na ngalawa yalioandaliwa na taasisi ya Tuna ambapo mshindi wa kwanza alipata tsh 400,000, wapili tsh 300,000 na wa tatu tsh 200,000.
Alisema serikali imesema inampango mkakati mzuri katika kuliendeleza sekta ya uvuvi kufika mbele zaidi ili sekta hiyo iweze kufanya vizuri na kusonga mbele zaidi
Meya alisema wavuvi wanapaswa kuwa wabunifu ili kusaidia sekta hiyo kufanya vizuri zaidi.