Mfahamu Mkuu wa kampuni ya uwakala aliye nyuma ya wachezaji wengi vijana wa Tanzania
Alex Morfaw ambaye ni Mkuu wa kampuni ya uwakala wa wanamichezo vijana kutokea Afrika inayojulikana kwa jina la Rainbow Sports iliyojikita katika kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana wa Afrika.
Alex Morfaw amejikita katika program za kutoa elimu za soka kwa vijana, mara kadhaa amekuwa akiihesabu Tanzania kwa bara la Afrika kama nyumbani kwake pia (second home) kutokana na kuwa muwakilishi wa wachezaji wengi vijana watanzania barani Ulaya kama wakala wao.
Inawezekana wengi hawafahamu lakini Alex Morfaw amefanikiwa pia kufanya kazi bega kwa bega na wakala anaetambulika na FIFA Kambi Zuberi kutoka @cambiassosports na ndio wakala nyuma ya vipaji vya wachezaji wakitanzania kama Ally Ng’anzi, Abdallah Shaibu, Theonasy Tepsi Evans, Onditi Samweli Jackson, Hamoud Nassor, Caminero Kapilima, Said Hamis na wengine wengi.
@alexmorfow @alexmorfow
@rainbow.sports @cambiassosports
#AlexmorfowinTz