Michezo
Mfalme wa Gofu Tiger Woods kurejea wiki hii
Mchezaji Gofu maarufu na mwenye mafanikio makubwa raia wa Marekani, Eldrick Tont “Tiger” Woods anatarajiwa kurejea tena katika mchezo huo kupitia michuano itakayofanyika Bahamas baada ya kuandamwa na majeraha kwa muda mrefu.
Woods mwenye umri wa miaka 41, anajumla ya mataji makubwa ya mchezo wa Gofu 14, huku akiwa ndani ya rekodi ya kuwa namba moja kwa takribani wiki 683 katika tasnia yake.
Woods kushudiwa wiki hii kupitia michuano ya dunia ya mashujaa (Hero World Challenge) itakayo fanyika huko Bahamas.