Habari
Mh. Mbowe aweka wazi alichokiona gerezani ‘Watu 1600 wanatumia vyoo vitatu'(+video)
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe ameweza wazi baadhi ya mambo aliyoyaona katika gereza la Segerea alilowekwa huku akieleza kuwa akiingia bungeni ataenda kuzungumzia watu kubambikiziwa kesi na hiyo ni moja ya hoja atakayoenda kuzungumzia bungeni.
Mbowe ameyasema hayo akiongea na wanachama wa chama hicho wa Mkoa wa Dar es Salaam Makao makuu ya Chama hicho yaliyopo kinondoni jijini Dar es salaam.