Habari

Mhe Lissu afunguka ishu ya kupima ‘haja ndogo’

Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), amefunguka jinsi maaskari walivyomkamata na kutaka kupima haja ndogo bila sababu maalumu.

Mhe Lissu amesema niliwakatalia kwa sababu nilishitakiwa kwa kosa la uchochezi na sio kosa lingine na kama wangemshitaki kwa kosa lingine linalomtaka afanye hivyo basi kisheria angefanya hivyo.

“Mimi nimeshtakiwa kwa uchochezi kupima mkojo, unadhibitisjhaje uchochezi na kupima mkojo? wakaniambia kuna vitu wanavitafuta, mimi nikawambia mkanishtaki na vitu hivyo kwanza ili muende kwa hakimu mkapate order ili mje mchukue mkojo wangu… anyway mimi niliwakatalia”,amesema Tundu Lissu kwenye mkutano wake na waandishi wa habari mapema leo baada ya kuachiwa kwa dhamana.

Hata hivyo Mhe Lissu amesema asingekubali kupima mkojo kwani kufanya hivyo angebambikiziwa kesi na kutengeneza headline kwenye magazeti.

By Godfrey Mgallah

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents