Habari

Mhe. Richard Kwitega awataka waajiri kuweka mifumo kuwalinda wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali maeneo ya kazi (+Video)

Katibu tawala Mkoa wa Arusha Mhe. Richard Kwitega amewasisitiza waajiri mkoani Arusha kuweka mifumo madhubuti ilikuwalinda wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali katika maeneo yao ya kazi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kwenye ufunguzi wa mafunzo maalumu ya Vision zero yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA) jijini Arusha, maalamu kwa wamiliki wa meoeo ya kazi mkoa wa Arusha, amesema uwepo wa mifumo mizuri maeneo ya kazi itasidia kuwakinga wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali zinazotokea maeneo ya kazi.

Ndugu Richard amesema wafanyakazi ni kipuri namba moja,kwa tassisi au kampuni yeyote katika ufanisi wakazi yeyote, amesema wafanyakazi wana mchango mkubwa sehemu ya kazi hivyo hawana budi kuhakikisha wanawalindwa dhidi ya magojwa na ajali zinazoweza kutokea sehemu za kazi, ilikuwawezesha kufikia malengo waliojiwekea.

Akiongea kwa niaba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Mkurugenzi wa Usalama na Afya mhandisi Alex Ngata amesema, Kampeni ya Vision Zero ni kampeni ya kidunia, nchi mbalimbali dunia nizinatekeleza kampeni hii, na lengo kuu la Vision zero ni kupunguza ajali na magonjwa sehemu za kazi.

Mhandisi Ngata amesema uwepo wa mfumo sehemu za kazi utawawezesha waajiri kujikagua wenyewe, na hivyo kuweza kuzuia magonjwa na ajali sehemu za kazi.

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo wamesema, Vision zero itawasaidia kwenda kuweka mifumo mizuri yakuwalinda wafanyakazi juu ya ajali na magonjwa sehemu za kazi, wamesema mafunzo hayo yamewajengea uelewa mpana juu ya masuala ya usalama na afya, vitu ambavyo walikuwa hawavifahamu.
CUE INN Diana Mamuya (Mshiriki wa Mafunzo) na Emmanual Mvamila

Vision zero ni Kampeni ya Kidunia iiliyoanzishwa kwa lengo ya kupunguza ajali na magonjwa sehemu za kazi,kampeni hiyo inazitaka maeneo ya kazi kuweka mifumo ya kuwalinda wafanyakazi dhidi ya magonjwa na ajali sehemu za kazi, na kampeni hii inatekelezwa kwenye mataifa mbalimbali duniani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents