Michezo
Michael Schumacher aanza kurejea kwenye fahamu zake
Michael Schumacher anadaiwa kujibu maelekezo ya madaktari walioanza kumrejeshea fahamu zake taratibu.
Mshindi huyo wa mara saba wa mashindano ya magari ya Formula 1 anadaiwa pia kuchezesha kope zake wakati akifanyiwa vipimo vya ubongo. Schumacher aliumiwa vibaya kichwani baada ya kuanguka na kujigonga kwenye mwamba alipokuwa akiteleza kwenye barafu huko nchini Ufaransa, December 29.
Tangu kipindi hicho, ameendelea kuwa katika hali ya kutojifahamu na amelezwa kwenye hospitali ya chuo kikuu cha Grenoble.