Michezo
Mikel Arteta kuondoka Arsenal majira haya ya joto
Nahodha wa klabu ya Arsenal Mikel Arteta anatarajiwa kuwa miongoni mwa wachezaji watakao hama klabu hiyo majira haya ya joto.
Arteta pamoja na kiungo wa kati mwenzake Tomas Rosicky wanatarajiwa kuondoka baada ya mikataba yao kumalizika.
Arteta, 34, alijiunga na klabu hiyo 2011 na amecheza mechi 150 na kufunga mabao 17.
Rosicky, 35, alijiunga na Arsenal 2006 na ameicheichezea Gunners mechi 246 kipindi cha miaka 10 wakati wa mechi yake ya mwisho dhidi ya Aston Villa Jumapili.
Arteta, aliyenunuliwa Everton kwa £10m, alionekana akitokwa na machozi baada ya mechi hiyo kumalizika.
Meneja Arsene Wenger amesema wachezaji hao wawili walikuwa wa kipekee.