Habari
Milioni 50 zamtoa Mhe. Zitto Kabwe mahabusu
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Mhe. Zitto Kabwe ameachiwa na Polisi kwa dhamana yenye thamani ya Tsh milioni 50 asubuhi hii mjini Morogoro baada ya kulala mahabusu tangu jana Alhamisi Februari 22, 2018 usiku.
Taarifa hizo zimethibitishwa na Wakili wa Mbunge huyo wa Kigoma Mjini, Ndg Emmanuel Mvula ambaye ndiye aliyemdhamini Zitto Kabwe na kusema kuwa anatakiwa kuripoti katika kituo kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro siku ya Jumatatu Machi 12, 2018.
Soma zaidi – Mhe. Zitto Kabwe anyimwa dhamana, Apelekwa mahabusu Morogoro
Mhe. Zitto Kabwe alikamatwa jana Februari 22, 2018 na Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro wakati akiwa katika ziara ya Chama cha ACT Wazalendo inayoendelea kufanywa na chama hicho katika mikoa 8 Tanzania bara.