BurudaniLady Jay Dee
Mimi ni mimi kuingia kwenye The Best of Lady Jay Dee
Mwanamuziki mkongwe wa muziki hapa nchini Judith Wambura ‘Jide’ ameshakamilisha wimbo wake wa Mimi ni mimi na Oliver Mtukuzi wa Zimbabwe. Mume na meneja wa mwanamuziki huyo Gadner G Habash amesema nyimbo hiyo imefanywa chini ya mkono wa Producer Man Water.
Ameongeza kwa kusema nyimbo hiyo imetungwa na Jide mwenyewe, huku ikiimbwa kwa lugha tatu tofauti ikiwemo Kiswahili , Kiengeleza na Kishona. Amesema nyimbo hiyo itakuwemo kwenye albamu ya Jide itakayozinduliwa Novemba ya The best of Lady Jay Dee.