Habari

Mimi ni sawa na wabunge 10 wa Chadema – Jerry Muro

Aliyekuwa Msemaji wa Yanga SC, Jerry Muro amesema kutokana na uwezo wake katika mambo mbali mbali anaweza kujilinganisha na wabunge 10 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Katika mahojiano na kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm, Jerry amesema kutokana na uwezo wake suala la ubunge kwake ni jambo rahisi tu sawa na kubofya button.

“Mimi Jerry Muro mmoja ni sawa na wabunge 10 wa Chadema, nimewazidi kifikra, kinguvu, kipesa, maadili, kihoja na mambo mengine mengi sana” amese Jerry.

Katika hatua nyingine Jerry amesema mwaka 2020 si ajabu kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Edward Lowassa wakirejea katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents