Burudani

Mimi ni tajiri ile mbaya yaani Bakhresa anasubiri! – Masanja Mkandamizaji

Mchungaji mjasiriamali, Masanja Mkandamizaji ameweka wazi kwamba ni kweli yeye ni tajiri kama baadhi ya watu wanavyosema kwenye mitandao ya jamii.

Akiongea na mtandao wa Clouds FM, Masanja amesema hawezi yakataa yale mazuri yanayozungumza na watu juu yake kwa kuwa midomo ya watu inanguvu sana.

“Kwa sababu ni jambo jema , unajua mtu akikwambia kuwa wewe unaoongoza kwa utajiri usikatae, ukikataa utakuwa umejikosea kwa sababu kitabu cha Mungu cha Biblia kinatufundisha nguvu iliyopo kwenye kinywa chako, kwahiyo mtu akisema kuwa mimi ni tajiri nitasema kuwa mimi ni tajiri ile mbaya na kwanini nisiwe tajiri wakati biblia inasema fedha na dhahabu ni mali ya baba yangu ninayemtumikia kwahiyo mimi kutumia au kumiliki vitu vya baba nimebarikiwa, ukiambiwa wewe ni tajiri usikae, ukikataa ina maana umeukataa utajiri’’ Alisema Masanja Mkandamizaji wakati akizungumza namtandao wa Clouds FM.

Aliongeza “Najisikia vizuri sana mtu akiniita tajiri na ulimi wangu lazima ukiri vitu vizuri kwahiyo ni kweli kabisa kama ambavyo wanasema mimi ni tajiri ile mbaya yaani Bakhresa anasubiri,” Aliongeza Masanja

Akizungumzia utajiri wake anaomiliki ikiwemo nyumba, magari ya kifahari na mashamba ya mpunga alisema:

‘’Nikwambie utajiri hautauhesabu kwa sababu ya kumiliki mjengo, ukimiliki mjengo ni sehemu tu ambayo Mungu amekubarikikwamba uwe unaweza kuwa na sehemu ya kuishi katikati ya watu wanaopanga, akikupa gari amekuhurumia tu kuepukana na mzunguko mingi ambayo ungetembea kwa miguu sasa unaweza kutumia usafiri kukurahisishia shughuli, utajiri wangu ni kuwa Yesu ambaye ana kila kitu, ukiwa na Mungu una kila kitu kwahiyo mimi ni tajiri zaidi matajiri kwa sababu nina kila kitu’’

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents