Burudani

Miss Burundi 16 wasusia shindano hatua ya fainali, mkwanja wahusishwa

Warembo 16, waliyokuwa wanashiriki shindano la kumtafuta Miss Burundi wamejiondoa katika hatua ya fainali na kutia hofu kupatikana kwa mlimbwende atakaye iwakalisha nchi hiyo kimataifa kwa mwaka huu wa 2018.

Kupitia barua waliyoandika walimbwende hao wamedai kuwa kunaudanganyifu mkubwa kwenye zawadi atakayotunukiwa mshindi wa kwanza na wapili.

Wandaaji wa shindano hilo awali walisema kuwa mshindi angejinyakulia gari jipya pamoja na kiwanja chenye ukubwa wa mita mraba mia nne na tuzo ya pesa taslim swala ambalo wasichana hao wanadai hakuna kilichoandalaliwa kwaajili yao mpaka sasa.

Fainali hiyo ambayo ilipangwa kufanyika tarehe 21 Julai 2018, ime ahirishwa na wandaaji wa shindano hilo na kusogezwa mbele hadi Julai 28.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents