Miss Kigamboni 2009
Vodacom Miss Kigamboni 2009 amepatikana Jumamosi iliopita, Karen Lukule
ameibuka mshindi na washindi wenzake ni Irene Christopher (kushoto)
ambaye alishika nafasi ya pili na Samirah Kapunda aliyeshika nafasi ya
tatu.
Shindano hilo liliandaliwa na Bongo5 Media Group na lilifanyika katika ukumbi wa Meese Beach Resort Kigamboni, majaji walikuwa Ben Kisaka (jaji mkuu), Miss kigamboni 2008 Lona Swai, Joketi Mwegelo ambaye alikuwa Miss Temeke 2007 na mdau Pinto kutoka Miss Tanzania UK.
Kwa upande wa burudani walianza na Barnabas & Pipi, akifuatia Maunda Zorro na kumalizia mtu mzima Marlaw.