Burudani

Miss Tanzania Kutoa msaada kwa Yatima Arusha

Genevieve

 

Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala, anatarajia  kutoa msaada kwa watoto yatima katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kama zawadi ya sikukuu ya Krisimas.

Genevieve ambaye anatarijia kuondoka jijini Desemaba 15, kuenda Arusha kwa shughuli hizo amesema tayari maandalizi yamekwisha malizika.

Aliongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa anatarajia kuondoka na warembo 12 ambao walishiriki mashindano ya urembo  mwaka huu ambao ni Glory Mwanga , Christine Justine, Consolata Lukosi, Bururi Ibrahimu, Wande Magese  Salma Mwakalukwa., wengine ni Anna Daudi, Asimu Malik, Furaha Davidd, Pendo Sam, Prisca Mkoyi pamona na Fatuma Ibrahimu.

Genevieve aliongeza kwa kusema kuwa  Mrembo wa mwaka 1997 Saida Kessy ndiye aliyefanya kazi ya kutafuta vituo vya watoto yatima  na kusema hii ni moja kati ya mikakati yake ya kufanya kazi za jamii katika kuwasaidia na kutoa msaada.

Awali Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya LINO Hashimu Lundenga  alisema jumla ya milioni kumi itatumika katika zoezi hilo ikiwa ni lengo la  kutimiza mipango ya  urembo wenye  malengo maalum.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents