Burudani
Mke wa Ludacris akunwa na wimbo wa Rich Mavoko aliyomshirikisha Patoranking ‘Rudi’ (+ Video)
Wimbo wa ‘Rudi’ wa Rich Mavoko ambao alimshirikisha msanii kutoka Nigeria Patoranking imemfikia mke wa msanii nyota wa Marekani ambae pia ni msanii na muigizaji Ludacris.
Mwanamama anayejulikana kwa jina la Eudoxie Mbouguiengue ambaye kupitia insta stories yake ameonekana akiimba wimbo huo uliotoka November 1, 2017. Eudoxie ni raia wa Gabon na alifunga ndoa Ludacris mwaka 2014, wana mtoto mmoja aitwaye Cadence.
By Ally Juma.