Burudani
Mkenya ala shavu kuhusika kwenye series maarufu ya Marekani, The Blacklist
Muigizaji wa Kenya, Edi Gathegi, amekula shavu la kuigiza kwenye msimu wa tatu wa series ya kimarekani, The Blacklist.
Gathegi alizaliwa Eastlands, Nairobi na kukulia California, Marekani.
Amewahi kuigiza kwenye filamu kubwa kama X Men, Twilight na House.
Kwenye msimu wa tatu wa series hiyo, Gathegi atakuwa upande wa maadui na atajulikana kama Mr. Solomon.