Burudani
Mkubwa na wanawe kuzindua kituo
Kundi la Mkubwa na wanawe wanatarajia kuzindua rasmi kituo cha muziki cha mkubwa na wanawe siku ya Mkubwa na wanawe Family day , pia watamtambulisha Dogo Aslay kwa wakazi wote wa Temeke na vitongoji vyake. Meneja wa kundi hilo Yusufu
amesema kwamba tamasha litafanyika kwenye ukumbi TCC Chang’ombe kuanzania saa nne asubuhi mpaka asaa nne usiku, siku ya tarehe 30 mwezi huu. Pia siku hiyo watazindua nyimbo mpya ya Tmk Wanaume family inayoitwa Kichwa kinauma, huku show zikiletwa kwenu na Diamond ‘Moyo wangu’ Suma lee ‘Hakunaga’ , Adam Mchovu ‘Baba John’, Tip Top Connection na kumaliziwa na Tht Dansa.