Habari

Mkuu wa Majeshi niletee majina yao haraka, sasa nimeona wakuwateua – Rais Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefurahishwa kuwaona wakuu wa Majeshi Wastaafu, Wanadhimu Wakuu wastaafu pamoja na wakuu wa JKT wastaafu katika uzinduzi wa Kituo cha Uwekezaji cha Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Rais Magufuli amesema kuwa amefurahishwa na viongozi hao wastaafu huku akisema kuwa na hata sura zao zinaonyesha kuwa bado ni vijana na wananidhamu.

“Nimefurahi kuwaona wakuu wa Majeshi Wastaafu, Wanadhimu Wakuu wastaafu pamoja na wakuu wa JKT wastaafu kujumuika nasi katika siku hii, hiki kimenifurahishwa sana na kila nilipokuwa nawaangalia wote vijana tu na nidhamu iko pale pale sasa nikuombe Mkuu wa Majeshi pamoja na Waziri wa Ulinzi niletee majina yao na mimi niwe nawakumbuka kumbuka hata kwenye Bodi mbalimbali kwasababu ni na uhakika, saa nyingine napata shida kuchagua wenyekiti wa Bodi, wajumbe Bodi ,” alisema Rais Magufuli.

Aliongeza “Yanaletwaga majina kule uadilifu wao unakuwa ni wa mashaka sana, lakini hawa ninavyowaona bado niwaadilifu vile vile kama walivyokuwa waadilifu katika kuongoza ulinzi na usalama niletee majina yao haraka ninashida nina Bodi nyingi sana za kuteuwa sasa nimeona wakuteua.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents