Burudani

Mkwanja wa dili la Voda ni ‘fifty fifty’ kati ya Diamond na Zari?

Wiki kadhaa zilizopita, Diamond Platnumz alisaini mkataba wa mamilioni ya shilingi kuwa balozi wa kampuni ya simu ya Vodacom Tanzania.

12558876_229434130733454_1488760884_n

Dili hilo limemfanya muimbaji huyo wa ‘Make Me Sing’ aonekane kwenye matangazo ya TV, yale ya barabarani, kwenye magezeti na vipeperushi vingine pamoja na kusikika kwenye matangazo ya redio.

Kwenye tangazo la TV, si Diamond pekee anayeonekana, bali familia yake nzima – wapo mpenzi wake Zari, mwanae Tiffah na mama yake. Lakini pia kuna tangazo moja la redio ambalo Zari anasikika akiwemo pamoja na Diamond na Mpoki.

Yeye mwenyewe Dangote alidai kuwa familia yake nzima ni brand na hilo halina ubishi. Lakini huenda Zari akawa anamega kipande kikubwa pia cha keki hiyo iliyotokana na mkataba wa Vodacom. Si jambo la kushangaza kwakuwa Mganda huyo sasa ni ubavu wa kushoto wa staa huyo na hakuna anayebisha kuwa mrembo huyo amekuwa akipush zaidi kampeni ya Ongea Deilee kwenye akaunti yake ya Instagram.

Lakini kibiashara, tunajua kuwa hata kama Zari ni mpenzi wake na Diamond mwenye ubalozi huo, na kwa ukubwa alionao, hawezi kupiga promo tu kwasababu anamsaidia mume wake. Yaani kwa mfano haijawahi kutokea Jay Z akimsaidia Beyonce kupromote kampeni za Pepsi kisa anamsaidia mke wake.

Kwanini? Kwasababu ni kila mmoja anasimama kama brand inayojitegemea. The same applies kwa Zari na Diamond. Na hivyo kwakuwa tunaona jinsi Mama Tiffah alivyo mstari wa mbele kupush kampeni hiyo, tunaanza kufikiria kuwa huenda wawili hao wamekula pasu mkwanja huo unaotokana na ubalozi wa Diamond – fifty fifty!

It’s good to be famous.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents