Habari

Mkwe wa Trump ambaye ni mshauri wa rais aanza ziara nchini Iraq

Mshauri mkuu wa rais Donald Trump ambaye pia ni mkwe wake Jared Kushner amefanya ziara nchini Iraq kwa mara ya kwanza wikiendi hii.

Afisa mmoja kutoka Ikulu ya Marekani ameiambia CNN kuwa Jared amesafiri na Jenerali Joseph Dunford katika ziara hiyo ambapo wanatarajiwa kurudi mapema wiki hii.

Siku chache zilizopita mshauri huyo na mkewe Ivanka Trump ambaye ameteuliwa kukalia kiti cha msaidizi wa rais asiyelipwa walitajwa kuwa na utajiri wa takribani dola milioni 740.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents