Michezo
Mlindalango wa Manchester United apata ajali mbaya ya gari
Mlindalango wa klabu ya Manchester United, Sergio Romero amepata ajali ya gari wakati akielekea kwenye kiwanja cha mazoezi cha Carrington.
Sergio Romero mwenye umri wa miaka 32, amepata ajali hiyo akiwa katika gari lake jeupe aina ya Lamborghini lenye thamani ya paundi, 170,000 ambayo sawa na shilingi milioni 510 za Kitanzania.
Hata hivyo taarira zinasema kuwa golikipa huyo mzaliwa wa Argentina hajapata majeraha kwenye ajali hiyo. Romero alijiunga na Manchester United mwaka 2015 akitokea klabu ya Sampdoria.