MMC: Top 20 ya Marimba Music Chart wiki hii (15th August 2013), Ommy Dimpoz aingia na Lady Jaydee aendelea kuonesha ukomando
Wiki hii katika Marimba Music Chart (MMC), chart rasmi ya muziki wa kizazi kipya Tanzania, Lady Jaydee aendelea kukaa kileleni huku Ommy Dimpoz na Young Killer wakiwa na maingizo mapya.
Lady Jaydee bado haoneshi dalili za kuiachia nafasi ya kwanza aliyoikamata kwa wiki ya nne mfululizo, huku Ommy Dimpoz na Young Killer wakifanikiwa kuingia na single zao mpya kama maingizo mapya wiki hii. Young Killer sasa anakuwa na nyimbo mbili kwa pamoja kwenye chart.
HII NDIO CHART RASMI YA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA WIKI HII
Ingia HAPA kupata Chart ya wiki iliyopita (8th August, 2013)
Marimba Music Chart huandaliwa na BONGO 5 kila wiki kutokana na Chart za Radio mbalimbali (zinazowakilisha radio zote) nchini.
VIGEZO:
MMC inatumia Chart za radio mbalimbali za Tanzania (sample) kuchuja na kupata orodha ya nyimbo zilizoingia katika chart nyingi zaidi na kupata nyimbo 20 (kwa sasa) ambazo ndio zinazofikia kigezo cha kuingia katika Marimba Music Chart.