Burudani
Mmoja ajitokeza kuzaa na Bieber
Mwanadada mmoja mwenye umri miaka 20 anaiyeitwa Mariah Yeater , amemshitaki mwanamuziki Justine Bieber mwenye umri wa miaka 17 kwa madai kwamba amezaa naye mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Tristyn.
Mwanadada huyo kwa kusaidiana na wakili wake Lance Rogers na Matthew Pare, walisema kwamba vipimo vya DNA, ndivyo vinavyothibitisha kwamba ni kweli mtoto huyo ni mwanamuziki huyo . Tayari mwanadada huyo ameshafikisha ushahidi, mahakamani kwaajili ya kuangalia nini kitafuata baada ya kutoa shutuma zake hizo, juu ya mwanamuziki huyo anayezidi kujizolea umaarufu mkubwa duniani.