Michezo

Mnyama ‘Simba SC’ amtafuna mwarabu ‘Al Ahly’ Taifa, sasa wanawinda pointi 3 muhimu kutoka kwa Wakongo ‘AS Vita’

Klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya waarabu Al Ahly kwenye mchezo wa klabu bingwa barani Afrika uliochezwa katika dimba la Taifa jijini Dar Es Salaam .

Goli la Simba limefungwa na Meddie Kagere kunako dakika ya 65 ya mchezo.

Kwa sasa Simba wapo nafasi ya pili kundi D wakiwa na pointi 6 huku Al Ahly akiongoza kundi hilo kwa alama 7.

Simba itahitaji alama tatu muhimu kutoka kwa AS Vita ya DR Congo, ili ijiwekee mazingira mazuri ya kufuzu robo fainali ya kloabu bingwa barani Afrika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents