Michezo

Mo Salah ashinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka PFA, Sane afanya kweli

Mchezaji hatari wa klabu ya soka ya Liverpool, Mohamed Salah ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka inayotolewa na Chama cha Wachezaji wa kulipwa nchini England (PFA).


                                             Mohamed Salah

Salah ameshinda tuzo hiyo kwa kuwabwaga wachezaji wengine akiwemo Harry Kane (Tottenham Hotspur), David De Gea (Manchester United), Kevin De Bruyne, David Silva na Leroy Sane (Manchester City).

Wakati huo huo Leroy Sane ameshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi wa soka nchini Uingereza. Sane amewashinda Sterling (Manchester City), Ryan Sessegnon (Fulham), Harry Kane (Tottenham Hotspur) na Marcus Rashford (Manchester United).


                                                  Leroy Sane

Kwa upande wa soka la wanawake, Fran Kirby (24) wa klabu ya Chelsea amefanikiwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa wanawake ya PFA.


                                                Fran Kirby

Naye Lauren Hemp wa Bristol City na timu ya wanawake chini ya umri wa miaka 19, amshinda tuzo ya mchezaji chipukizi kwa upande wa wanawake.


                                            Lauren Hemp

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents