Michezo

Mo Salah rasmi kushiriki kombe la dunia Urusi

Uongozi wa timu ya Taifa ya Misri umethibitisha kuwa mshambuliaji wao hatari amabye anacheza kwenye klabu ya Liverpool, Mohamed Salah atashiriki kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi itakayoanaza kufanyika Juni mwaka huu.

Salah ambaye aliumia bega la kushoto wakati wa fainali ya klabu bingwa ya Ulaya Jumamosi iliyopita baada ya kuchezewa vibaya na Sergio Ramos na kutoka nje yauwanja dakika ya 24.


Sergio Ramos akimchezea rafu mbaya Mohamed Salah

Kutokana na majeraha hayo yalileta wasiwasi kwa mashabiki na kuhusu kushiriki kwake kwenye michuano hiyo mikuba ya dunia.

Wakati huo huo Mwanasheria wa Misri, Bassam Wahba amesema amepeleka kesi kwenye shirikisho la soka duniani (FIFA) kumshtaki Ramos atoe kiasi cha Euro billion moja kwa kumuumiza makusudi Salah.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents