Mobby Mpambala na filamu za Action
Mwigizaji wa filamu za Action, Mobby Mpambara, amesema ingawa ni msanii mzuri wa filamu na anafanya vizuri lakini hatoweza kuidharau kazi yake ambayo imemtoa mbali. msanii huyo alisema watu wengi wamekuwa wakishindwa kutaja kazi zao lakini yeye yupo tofauti sana.
Aidha amedai hawezi kuficha chochote kuhusu maisha yake, na kazi yake iliyomlea katika maisha yake. pia amesema watu wengi wamekuwa wakishangazwa na maisha anayoishi kutokana na Usiliasi anaounyesha kwenye filamu na maisha yake harisi.
Aidha Mobby amesema, watu wamekuwa wakimwogopa kutokana na kuzoea kuigiza filamu za Action, hususani za kijambazi na ukatiri wa hari ya juu.
Mtoto wa Mobby wa kwanza yeye ni tofauti na baba yake, kwani anapenda sana filamu za Comedy, na anatarajia kuja na filamu zake na vichekesho
Mobby Mpambala, akiwa kwenye makaratasi ambayo yanaonyesha baadhi ya filamu alizoigiza, ikiwemo My Brother, She Dead, na nyingine nyingi