Michezo
Mohamed Salah aingia kandarasi ya muda mrefu Liverpool
Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool, Mohamed Salah ameingia kandarasi ya muda mrefu zaidi ndani ya timu hiyo baada ya kuitumikia kwa mafanikio makubwa msimu uliyopita.
Salah mwenye umri wa miaka 26 raia wa Misri ameamua kusaini muda mrefu baada ya kuipatia mabao 44 kwenye michezo 52 aliyocheza na sasa atakuwa anaingiza pauni 200,000 kwa wiki kiasi ambacho kinamfamnya kuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi katika historia ya klabu hiyo.