Michezo

Morgan Schneiderlin akaribia kutua Everton, afanyiwa vipimo Ijumaa hii

Imedaiwa kuwa Ijumaa hii mchana kiungo wa klabu ya soka ya Manchester United, Morgan Schneiderlin ameonekana kwenye kliniki ya kufanyia vipimo vya afya ya Finch Farm ili kujiunga na Everton.

Mchezaji huyo ambaye alisajiliwa na United msimu uliopita kwa dau la paundi milioni 25 akitokea Southampton, atajiunga na Everton kwa dau lisilopungua paundi milioni 20 hiyo ni kwa mujibu wa taarifa za vyombo mbalimbali vya habari vya Uingereza.

Schneiderlin ameonekana kukosa namba kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Jose Mourinho tangu alipowasili kwa ajili ya kuifundisha timu hiyo tangu msimu huu ulipoanza. Mpaka sasa mchezaji huyo ameshaichezea Man United jumla ya mechi 47 tangu aliposajiliwa huku akianza katika mechi 36 na nyingine 11 akitokea benchi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents