Habari
Most Expensive Dog: Mbwa anunuliwa kwa tshs bilioni 3.2 nchini China
Mbwa wa huko nchini China amenunuliwa kwa dola milioni 2 (sawa na zaidi ya shilingi bilioni 3.2) na kufanya kuwa mbwa aliyenunuliwa kwa bei kubwa zaidi.
Kwa mujibu wa Qianjiang Evening News, mbwa huyo alinunuliwa kwa Yuan milioni 12 mashariki mwa jimbo Zhejiang. Mbwa hao wanadaiwa kufanana na simba na wana thamani kubwa kwakuwa wanaaminika kuleta bahati, afya na ulinzi.