Mourinho: Kwa mtazamo wangu, timu bora imeshindwa (Manchester United)
Pamoja na Real Madrid jana kuwafungashia virago Manchester United kwenye ligi ya mabingwa wa Ulaya na kuingia robo fainali, kocha wa Real Jose Mourinho, ameipongeza Man U kwa mchezo mzuri waliouonesha na kudai kuwa walistahili kushinda.
Mourinho amesema kwa mtazamo wake timu bora ndio iliyoshindwa na kwamba kama Man wasingepata kadi nyekundu wangeshinda. Amesema refa wa mchezo huyo alipaswa kumpa kadi ya njano Luís Nani kwa kumchezea ndivyo sivyo Álvaro Arbeloa na sio kadi nyekundu.
Cristiano Ronaldo hakuionea huruma timu yake ya zamani baada ya kufunga goli lililoiwezesha Real Madrid kusonga mbele.
Magoli ya mawili ya Real Madrid yalifungwa na Luka Modric na Ronaldo baada ya United kuanza kuongoza kwa goli moja ambalo Sergio Ramos alijifunga. Kutokana na matokeo hayo, kocha wa United Alex Ferguson alikasirishwa na uamuzi wa refa Cuneyt Cakir kiasi cha kukataa kuongea waandishi wa habari na kumwachia msaidizi wake Mike.