Michezo
Moyes amtisha Ferguson
Kocha wa Everton,David Moyes amemshtua kocha wa Man United,Alex Ferguson baada ya kutangaza nia yake ya kumtaka Federico Macheda.
Moyes anataka kumchukua mchezaji huyo kwa mkopo lakini swala hilo litakua gumu kwa Ferguson ambaye anaona kiwango cha mchezaji huyo kinapanda kwa sasa licha ya kutompa nafasi katika kikosi cha kwanza.
Limefahamika kwamba iwapo atamkosa kwa mkopo basi Moyes atatangaza dau la kumsajili Januari mwakani.
Lakini habari kutoka Man United zinasema,Macheda anashauku ya kuondoka katika klabu hiyo ili apate nafasi ya kwanza kwani kwa sasa anacheza nyuma ya Rooney, Berbatov na Hernandez (Chicharito