Burudani

Mpenzi wa Justin Baiber, Hailey Baldwin apata baraka za Mama Mkwe “Ni kama zawadi kwa mwanangu”

Licha ya harusi ya wawili hawa Justin Baiber na Hailey Baldwin kupangwa kufanyika rasmi mwezi kwa taarifa kutoka kwa watu wa karibu na familia hizo mbili kwani, tayari wanaonekan wameshaanza kuwatumia watu wao wa karibu kadi za mwaliko.

Mtandao wa Pagesix umeripoti kuwa mipango yote ya harusi imeshakamilika na maandalizi yanaendelea ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa urembo, madensa pia wameshaanza mazoezi na Dj wa Bieber mwenyewe, Dj Tay James ndio ata’dj kwenye harusi.

Harusi hii inakuja licha ya Bieber na Hailey kufunga ndoa ya kisheria tangu mwezi Septemba mwaka jana na tayari wameshaanza maisha yao ya ndoa, hivi karibuni kwani pia walionekana wakitafuta nyumba ya pamoja kwenye mitaa ya Los Angeles, huko Marekani.

Lakini hayo yakiendelea mama mzazi wa msanii Justin Baiber amefunguka na kusema kuwa “mkwe wake huyo yaani mpenzi wake Justin Hailey ni kama zawadi kwa mwanae”

Maneno hayo aliyaandika kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusema ” What a gift”

Mbali na kusema hivyo lakini pia alishawahi kuongea na kusema

“Justin na Hailey wanafurahi sana mapenzi yao na hawawezi kutenganishwa,” Kwani wamekuwa wakionyesha mapenzi yao hadharani pia kwa marafiki zao hadi kufikia kwa familia zao” mtandao wa ET ulisema.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents