Mrema asafishwa na wenzie
Naibu katibu mkuu wa TLP, Hamad Rajab Tao leo amezindua kitabu kinachoelezea undani wa mvurugano unaoendelea katika chama hicho kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari maelezo. Kwenye kitabu hicho, katibu ameelezea kashfa zinazomuandama Mwenyekiti wa taifa wa TLP. Ndg Augustine Mrema na kusema kwamba hazina ukweli wowote. Miongoni mwa kashfa hizo ni kubinafsisha nyumba ya chama na kutumia shilingi milioni 15 kununua nyani wa Kampeni
Aidha, naibu katibu mkuu huyo ambaye aliwahi kusimamishwa uanachama wa
chama hicho kwa muda amesema kwamba lengo la kuandika kitabu hicho si
kujikosha kwa mwenyekiti wake bali kusukumwa na uzalendo baada ya
kufanya utafiti wa takribani miaka 4