Burudani

Mrembo Alicios ashindwa kujizuia kimahaba kwa Idris Sultan ‘nipo single nitadata, naomba anipokee nakuja Tanzania’

Msanii wa muziki kutoka DR Congo ambaye kazi zake anafanyia nchini Kenya, Alicios Theluji ameshindwa kujizuia na kutangaza kuwa kwa sasa hakuna mwanaume anayempenda zaidi ya Idris Sultan.

Image result for alicious
Alicios

Alicios akizumngumza kwenye kipindi cha Mseto East Africa cha Radio Citizen amesema kuwa Idris ni Crush wake lakini pia ni mtu ambaye anampenda sana.

Kwa sasa nipo single, Idris nina Media Tour hivi karibuni nakuja Tanzania naomba unipokee Airport.” ameeleza kwa hisia Alicious na kutaja vigezo vya mwanaume anayempenda kwa kusema “Navutiwa sana na mabega nadata, umeshawahi kuona mabega ya Idris wewe?

Mrembo huyo pia amefunguka kuwa licha ya kuwa kwenye mahusiano ya muda mrefu, ila kwa sasa ameachana naye kutokana na sababu za hapa na pale.

Kwa sasa Alicios ameachia ngoma mpya inaitwa NADATA unaweza ukaisikiliza hapa chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents