Michezo

Mrembo apokea kipigo kibaya Ulingoni, Mchina amuaribu jicho mwenyewe adai hajakata tamaa 

Nyota wa mapambano ya ‘The Ultimate Fighting Championship’ (UFC),  Karolina Kowalkiewicz amesema kuwa huwenda akang’atuka na kuachiliambali mchezo huo hii ikiwa ni baada ya kuchezea kichapo kibaya ulingoni kutoka kwa Mwanadada wa raia wa China, Xianon Yan Februari 22, 2020 kilichopelekea kufanyiwa upasuaji mdogo wa jicho.

The Pole was on the receiving end of some vicious shots by her opponent Xionan Yan

Kupitia akaunti yake ya kijamii ya Instagram, Kowalkiewicz amewashukuru mashabiki zake kwa kuendelea kuonyesha ushirikiano katika kipindi chote ambacho yupo kwenye matibabu huko Warsaw, Poland.

Mwanadada huyo raia wa Poland amepata jeraha jichoni na sehemu nyingine ya uso wake baada ya kuchezea kipigo na kujikuta anapoteza pambano lake dhidi ya, Yan ‘UFC Fight Night Auckland’ na anatumaini hilo sio pambano lake la mwisho katika Mixed Martial Arts.

”Natumai hhuu sio mwisho wa kupambana, lakini kwa sasa natazamia juu ya afya yangu. Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu baada ya pambano siwezi kusema nipo salama, kama unavyoweza kuona mwanzoni mwa raundi ya kwanza niliharibika baadhi ya vishipa na kushinda kuona vizuri.” Amesema kwa hisia mwanadada huyo mwenye umri wa miaka 34.

Kowalkiewicz last week posted an emotional video describing what happened in Auckland

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents