Mrithi wa Maximo
Kocha muingereza Stewart Hall ameielezea nia yake ya kurithi mikoba ya Mbrazil Marcio Maximo kuinoa Taifa Stars. Hall, ambaye ameshawahi kuzifundisha timu za taifa za Trinidad & Tobago na St. Vincent & Grenades na klabu ya India ya Pune FC, amesema hivyo kupitia Uk Press huko ikiwa imebaki miezi michache mkataba wa Maximo kumalizika na amesisitiza umuhimu wa kuwanoa makocha wazalendo ili kuinua soka nchini
Kocha huyo ameshawahi kuja nchini mara mbili, mara ya kwanza ikiwa mwaka 2006 na 2007 akiwa na wachezaji wa zamani wa Uingereza John Barnes na Les Ferdinand na ameshawahi kuandika mada ya ‘Team Tanzania’