Burudani

Msanii Chester Bennington afariki dunia kwa kujiua

Msanii wa muziki kutoka Marekani, Chester Bennington amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 41.

Chester alikutwa amefariki dunia akidaiwa kujinyonga mwenyewe nyumbani kwake Palos Verdes Estates mjini Los Angles. Muimbaji huyo wa Linkin Park pia alikuwa na urafiki wa ukaribu na Chris Cornell amabye na yeye alijiuwa mwezi Mei mwaka huu kwa kuzidisha madawa.

Joe Hahn DJ wa kundi la Linkin Park akielekea msibanit

Chanzo cha kifo cha Chester kimeelezwa kuwa marehemu alikuwa akinyanyaswa na mwanaume mmoja hali iliyokuwa ikimpelekea kujiona kama mtoto.

Kifo hiko kimetokea wakati kundi la Linkin Park, likijiandaa kwenda kufanya photoshoot mjini Hollywood kwa ajili ya wimbo wao mpya. Marehemu ameacha watoto sita aliokuwa amezaa na wanawake wawili tofauti, pia inaelezwa msanii huyo alikuwa akitumia madawa ya kulevya pamoja na pombe kali.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents