Msanii huyu wa Nigeria atamani kufanya kazi na Harmonize
Kufanya kwake kazi chini ya Diamond Platnumz anayetazamwa zaidi kwa sasa ndani na nje ya bara la Afrika, kumemfanya Harmonize naye kuanza kufata nyayo za boss wake kimafanikio.
Licha ya kuwa Harmonize ni msanii mpya lakini promo kubwa anayoipata kwenye vituo vya nje ikiwemo Nigeria vimemuweka kwenye nafasi hata ya kufikiriwa kufanya kazi na wasanii wa huko.
Kiss Daniel
Msanii wa Nigeria, Kiss Daniel ndiye aliyeonesha nia ya kutaka kufanya kazi na mumbaji wa ‘Aiyola’ baada ya kuulizwa Twitter kama ana mpango wa kufanya collabo na msanii yeyote wa Tanzania.
“Diamond of cuz .. Tho I love this new dude signed to his label” alijibu Kiss Daniel.
Diamond of cuz .. Tho I love this new dude signed to his label https://t.co/to7dzWDW34
— KISS DANIEL (@iamkissdaniel) January 7, 2016