Burudani

Msanii mkongwe wa Afrika Kusini afariki dunia

Tasnia ya muziki nchini Afrika Kusini imekumbwa na majonzi kwa kumpoteza Hugh Masekela ambaye alikuwa mpiga trumpeter mkongwe nchini humo.


Hugh Masekela enzi za uhai wake

Masekela amefariki Jumanne hii akiwa na umri wa miaka 78 kwa maradhi ya saratani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia yake imesema, “Baada ya vita vya muda mrefu na ujasiri na saratani ya kinga, amefariki kwa amani huko Johannesburg, Afrika Kusini, akizungukwa na familia yake.”

Naye Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma ametuma salamu zake za rambi rambi kwa familia ya marehemu kwa kusema, “Taifa linaomboleza kipaji kimoja kinachojulikana zaidi … Ni kupotea kabisa kwa sekta ya muziki kwa nchi nzima. Mchango wake katika mapambano ya ukombozi kamwe hauwezi kusahaulika.”

“Tunataka kufikisha matumaini yetu ya moyo kwa familia yake na wenzake katika ushirika wa wasanii na utamaduni kwa ujumla. Na nafsi yake ipumzike kwa amani,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents