Burudani

Msanii wa miaka 21 afariki dunia kwa ajali mbaya Ghana

Msanii kutoka nchini Ghana Priscilla Opoku Kwarteng maarufu kwa jina la Ebony Reigns, amefariki dunia katika ajali mbaya ya gari.

Ajali hiyo imetokea katika barabara ya Sunyani-Kumasi, Brong Ahafo. Kwa mujibu wa jeshi la polisi nchini humo limesema mrembo huyo (21) alikuwa kwenye gari aina ya Jeep 4×4, lenye namba za usajili AS 497—16.


Moja ya picha zilizopigwa kwenye ajali hiyo

Polisi hao wameongeza kuwa katika ajali hiyo watu wengine wawili waliokuwepo kwenye gari la msanii huyo ambao wanadaiwa ni wanajeshi wamefariki dunia walipofikishwa katika Hospital ya Mankranso.

Muimbaji huyo kwenye mtandao wake wa Instagram alikuwa anatumia jina la ebony_reigns na watu takribani 285k walikuwa wame-mfollow.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents