Burudani

Mtanzania Emanuel Austin na mkewe wanavyosherehekea mafanikio ya mwaka 2017 barani Asia

Hakuna kitu kizuri kama kufanikiwa katika kile ulichokipanga. Emanuel Austin ameamua kusherehekea mafanikio aliyoyapata katika mwaka 2017 baada ya ndoto zake za kuandaa matamasha matatu makubwa nchini Ujerumani kufanya vizuri.

Austin ameamua kusherehekea mafanikio hayo kwa kufanya ziara katika bara la Asia akiwa na mkewe Larissa Bertsch ambapo wote wanamiliki chuo cha Tanzschule Weiss kilichopo katika mji wa Frankfurt.

Katika matamasha yalilofanyika mwezi Septemba na Novemba katika ukumbi wa chuo hiko watu takribani 10,000 walihudhuria, na katika tamasha la mwezi Disemba watu zaidi ya 11,000 walifanikiwa kuhudhuria. Hizi ni picha nyingine za Austin na mkewe Larissa wakisherehekea barani Asia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents