Michezo
Mtoto wa mchezaji Rivaldo aihama timu ambayo baba yake ni Rais
Mtoto wa mchezaji wa zamani wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Brazil ambaye pia aliwahi kuwa mchezaji bora wa duniani, Rivaldo aitwaye Rivaldinho anayeonekana kufuata nyayo za baba yake katika soka amesajiliwa na klabu ya Boavista ya Ureno akitokea klabu ya Mogi Mirim ya kwao Brazil.
Rivaldinho mwenye umri wa miaka 20 amesajiliwa na klabu ya Boavista kwa mkataba wa miaka mitatu na hivyo inamfanya kuwa mbali na baba yake aliyekuwa rais wa klabu ya Mogi Mirim.