Uncategorized
Mtoto wa mchezaji wa zamani wa Simba aiwezesha Qatar kutwaa ubingwa wa Asian Cup, atupia moja kati ya mabao ya ushindi
Mshambuliaji wa timu ya Qatar, Akram Hassan Afiff ambaye ni mtoto wa nyota wa zamani wa klabu ya Simba, Hassan Afiff ameliongoza taifa hilo kutwaa ubingwa wa Asian Cup dhidi ya Japan kwa jumla ya mabao 3 – 1.
Akram alifanikiwa kufunga bao moja kwa njia ya mkwaju wa penati huku akitoa pasi za mwisho zilizozalisha magoli hayo mawili na kufanya kuibuka na ushindi wa mabao 3 – 1.
Mtoto wa mchezaji wa zamani wa Simba aiwezesha Qatar kutinga nusu fainali Asian Cup
Kwenye michuano hiyo Akram ameweka rekodi ya kupika jumla ya mabao 10 fainali ikiwa imefanyika Abu Dhabi.
Akram mwenye umri wa miaka 22 ni Mtoto wa kiungo na kocha wa zamani wa Simba, Hassan Afif.