Burudani
Mtoto wa miaka 8 atikisa kwenye Britain’s Got Talent
Mtoto Issy Simpson mwenye umri wa miaka nane ameshangaza ulimwengu katika mashindano ya Britain’s Got Talent kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufanya mazingaombwe.
Issy amefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali Jumapili hii baada ya kufanya vizuri katiuka hatua ya nusu fainali ya pili ambapo alikuwa akishindana na washiriki wengine saba.
“Congratulations to winner Issy Simpson and runner-up Matt Edwards, you’re both through to Sunday’s Live #BGT Final! ?,” wameandika katika mtandao huo.
Kupitia mtandao wa Instagram, waendesha mashindano hayo wamempongeza mtoto huyo kutokana na uwezo wake ambapo fainali hiyt itafanyika Jumapili ya Juni 5.