Burudani

Muigizaji wa Kuch Kuch Hota Hai afariki

Reema Lagoo, muigizaji mkongwe kutokea nchini India aliyekuwa akiishi katika mji wa Mumbai amefariki dunia kwa kuugua kifua.

Lagoo amefariki akiwa katika hospitali ya Dhirubhai Ambani, masaa machache baada ya kufikishwa hospitalini hapo. Marehemu amepata umaarufu kupitia filamu ya “Kuch Kuch Hota Hai”, Kabla ya umauti wake amekuwa akigiza mara nyingi kama mama kwenye filamu kama vile “Hum Aapke Hain Koun” na “Kal Ho Na Ho”.

Lagoo mwenye miaka 59 kabla mauti kumfika, alifikishwa hospitalini hapo lakini alikuwa akilalamika juu ya maumivu makali ya kifua, Alisema msemaji wa Hospitali hiyo Bw. Ram Naraian.

Kabla ya mauti kumfika, marehemu amewahi kuigiza filamu kama vile “Maine Pyar Kiya”, “Saajan”, “Vaastav, na “Hum Saath-Saath Hain”., pia alikuwa akionekana kwenye tamthilia iitwayo “Naamkaran”, inayooneshwa Star Plus.

Na Laila Sued

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents